Huduma ya mtoto na maendeleo ya kijana inafanya maadhimisho ya miaka 25 ya kuanzishwa kwa huduma hiyo | Extra Mile

Tuesday, April 23, 2024

Huduma ya mtoto na maendeleo ya kijana inafanya maadhimisho ya miaka 25 ya kuanzishwa kwa huduma hiyo

  Extra Mile       Tuesday, April 23, 2024

 Wakati Huduma ya Maendeleo ya Mtoto na Kijana wilayani Kahama mkoani Shinyanga ikiadhimisha miaka 12 tangu kuanzishwa kwake Wilayani humo ikiwa ni miaka 25 tangu kuanzishwa kwa huduma hiyo nchini Tanzania, Huduma hiyo imeiomba serikali kupewa nafasi na kutambuliwa katika vyuo vya serikali


Akitoa Risala mbele ya mgeni Rasimi mwenyekiti wa vijana Daudi Mathiasi  amesema kuwa malengo ya Huduma hiyo ni kuwasaidia watoto katika malezi ya kidini, kuwasaidia watoto hao wanaishi katika mazingira magumu ya ki

Katika hatua nyingine mwenyekiti huyo ameeleza changamoto inayoikabili huduma hiyo ikiwa ni changamoto ya kukosa nafasi katika vyuo vya serikali ambapo wameiomba Halmashauri hiyo kuwatambua na kuwawezesha katika kipindi cha vyuo 


Katika kujibu risala hiyo Mgeni Rasmi bi Swahiba Chem chem ambaye ni Afisa Maendeleo na Ustawi wa Jamii manispaa ya Kahama akimuwakilisha Mkurugenzi wa manispaa ya kahama ameeleza kuwa Halmashauri ina ufadhiri wa wanafunzi wa vyuo vya kati na vyuo vikuu hivyo waainishe watu wanaohitaji ufadhili na kuwasilisha Halmashauri kwa ajili ya usaidizi



Baadhi ya vijana ambao ni zao la shirika hili wamesema kuwa shirika hili limewajengea uwezo kupitia fani mbali mbali ikiwa ni pamoja na upigaji picha, ushonaji wa nguo, pamoja na upakaji rangi ambazo zinawasaidia kujiingizia kipato

Huduma ya mtoto na maendeleo ya Kijana Tanzania inaratibiwa na  Shirika la compassion Tanzania ambapo kwa kahama limetimiza miaka 12 na linahudumia watoto takribani 1200 wilayani Kahama.





logoblog
Previous
« Prev Post
Oldest
You are reading the latest post