WAZIRI MKUU: MATOKEO YA SENSA YAWAFIKIE WATENDAJI WOTE WA MIKOA NA HALMASHAURI | Extra Mile

Tuesday, July 2, 2024

WAZIRI MKUU: MATOKEO YA SENSA YAWAFIKIE WATENDAJI WOTE WA MIKOA NA HALMASHAURI

  Extra Mile       Tuesday, July 2, 2024

 





WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema matokeo ya sensa yanapaswa yawafikie watendaji na walengwa wote katika ngazi ya mkoa na Halmashauri na yawe msingi wa rejea katika kufanya maamuzi yote ya kibajeti, kupanga miradi ya maendeleo na kufuatilia utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya kisekta.

Ametoa agizo hilo leo (Jumanne, Julai 2, 2024) wakati akizungumza na viongozi, wananchi na wadau mbalimbali waliohudhuria ufunguzi wa Mafunzo ya Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 kwa Viongozi na Watendaji wa Halmashari za Wilaya za Liwale, Nachingwea na Ruangwa mkoani Lindi uliofanyika kwenye viwanja vya Maonesho, Kilimahewa mjini Ruangwa.









logoblog
Previous
« Prev Post