Profesa wa sheria na mwanadiplosia Profesa Costa Mahalu (77) amefariki dunia.
Taarifa kutoka kwa familia yake imethibitisha kwamba Profesa Mahalu amefariki dunia leo Jumatatu Machi 9, 2026 katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) alikokuwa akipatiwa matibabu.
Alitambuliwa kama msomi mahiri, mwalimu mchapaji kazi, na mwanadiplomasia mwenye uzoefu, aliyesaidia Tanzania kukuza elimu ya sheria na kuimarisha uwakilishi wake kimataifa.
Profesa Mahalu alizaliwa Julai 9, 1948, katika Kijiji cha Katunguru, wilayani Sengerema, Mkoa wa Mwanza.
